MR KAPAMA`S LIFE


MAISHA YA MR DENIS KAPAMA
Mr Denis Kapama alizaliwa mnamo tarehe 28/12/1964. katika kijiji cha  jelemanga. wilaya ya Mpanda Zamani mkoa wa Tabora baadaye Rukwa na sasa ni Katavi akiwa ni mtoto wa saba katika familia ya watoto kumi na mbili wa Mzee Vitalis Kapama na Bi Juliana mucodemu Kisaye. Mr Denis kapama alibatizwa katika kanisa la parokia ya milala mnamo mwaka 1965. Alipata mafundisho ya komuniyopamoja na kipaimara.
 Mr Denis kapama alianza safari yake ya kutafuta elimu mnamo mwaka 1977 mpaka 1983.Alipo hitimu elimu yake ya msingi katika shule Kasokola pia akajiunga na elimu ya sekondari  kuanzia mwaka 1984 mpaka katika shule ya sekondary Kantalamba High School. Alijiunga na kidato cha sita {A-level} mwaka 1988 mpaka 1990 katika shule ya sekondari  Sengerema High School mnamo mwaka 1990.Baada ya hapo Mr Kapama alijiunga na jeshi la kujenga Taifa {JKT} kwa mujibu wa sheria katika kambi ya jeshi ya Itende mkoani Mbeya na kumalizia mafunzo yake makao makuu ya JKT mlalakuwa  Kawe jijini Dar es salaam.Akajiunga na elimu ya juu katika chuo kikuu cha Dar es salaama kuanzia mwaka 1993 na kuhitimisha shahada  ya uwalimu mnamo mwaka 1997.

                  Mda wote huwo Mr Kapama alikua akijisomesha uku akifundsha shule ya aga khan. Mwaka 2010 mpaka 2012  Mr Kapama alipata alipata shahada ya Uzamili ya uwalimu {Masters of Education} katika chuo kikuu cha Dar es saalam,Mwaka 2013 mpaka 2015 alitunukiwa shahada ya kwanza ya Sheria katika chuo kikuu cha Bagamoyo University,vilevile Mr Kapama kwa juhudi zake za kusoma alitunukiwa tena shahada uzamili ya sheria {Masters of Laws} katika chuo cha Bagamoyo University mnamo mwaka 2013 mpaka 2015.

Mr Kapama aliajiliwa katika shule ya sekondari ya Aga Khan Mzizima,Mnamo mwaka 1997 mpaka 2000. Mwaka 2000 aliajiliwa katika shule ya Dar es salaam Independent  International School iliyopo Mikocheni katika jiji la Dar es salaam ambapo alidumu kwa miaka michache. Mwaka 2002 Mr Kapama aliamua kujiajili mwenyewe kwa kuanzisha kituo cha elimu ya watu wazima na ushauri nasaha cha TANGANYIKA EDU-CONSULT CENTRE {TECC} ambacho kilianzishwa maeneo ya mwenge na baadae kuhamia sinza mori na sasa kituo hiko kipo  survey. Alikuwa ndio mkuu wa kituo hiko pia mwalimu wa baadhi ya masomo ambayo nayo ni English Language, Literature, General Studies  pia na Geography. Mr denis pia alikua vile vile akiwa ni mlezi mlezi wa PAN AFRICANISM,Tanganyika chapter na  mchambuzi wa vipindi mbalimbali vya redioni pia kwenye luninga kama vile E-FM  na CLOUDS FM  kama mtaalam wa sheria na maswala ya kijamii.

Mr Denis Kapama aliishi vizuli na jamii yote iliyo mzunguka na alikuwa amejaliwa moyo wa huruma na kujitolea katika kusaidia watu wenye shida/uhitaji vilevile alijitoa kwenye kutoa elimu na kuzalisha wasomi wengi hata wale waliokua wamekata tamaa ya kupata elimu aliwezakuwatia moyo  na kuwasaidia kupata elimu mchango huo mkubwa umekuwa chachu kubwa ya maendeleo kwa jamii inayo mzunguka na Taifa kiujumla. Mr Denis alikuwa mstari wa mbele katika kupigania haki na uongozi bora kwa kutoa elimu ya kijamii kwa watu wote waliomuhitaji na waliomzunguka .

Mr Denis Kapama alifunga ndoa na Rose Chuku mnapo mwaka 12/7/1997 katika kanisa la St.Joseph, liliopo posta jijini Dar es saalam  na kubalikiwa kupata watoto wanne wote wakiume nao ni Vitalis,Kisaye,Joseph na Afrika .

Mr Kapama alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kisukali kuanzia mwaka 2009 katika muda wote huo wa ugonjwa Mr Kapama akipata tiba katika hospitalize MUHIMBILI ,CCBRT  na TUMBI kwa kipindi chote hicho aliendelea kuimarika kiafya kwa kuzingatia matumizi sahihi ya dawa , Tiba na ushauri kutoka kwa madaktari mnamo tarehe  12/1/2020 .

 Mr Kapama alikuwa na furaha. Ilipofika jioni aliwaambia watoto wake wote wanne pamoja na mtoto wa shemeji yake wakae kikao ili kujadili mapungufu yao. Nao watoto kwa nidhamu ya juu walitii walikaa kikao na kukosoana mabaya na kuchekeshana. Mr kapama alivoona hivo aliwanunulia soda watoto wote. Baada ya mda kidogo alianza kulalamika kwamba kifua kinamuuma. Usika wa saa nne alikimbizwa hospitali na kuchomwa sindano baada ya hapo alirud nyumban na kupumzika kwa nje akiwa na mke wake,shemeji yake watoto wake wawili Kisaye na Jose pia na Fauster mtoto wa shemeji yake . Alikuwa akicheka nao na ghafla mida ya saa saba usiku Mr Kapama alifaliki mbele ya Familia yake.walijitahidi kumuwahisha hospitali lakini MUNGU alipenda Mr Denis Kapama apumzike kwa amani tangu usiku huo wa tarehe 13/1/2020.

Post a Comment

3 Comments

Unknown said…
Well written, we got you friends, may his soul rest in eternal peace over all times Amen!