TOSC 2024


 


Kituo Cha Elimu na Ushauri ChaTanganyika

(Centre of Counselling and Academic Excellence)

 

UTANGULIZI

Kipeperushi hiki kina lengo la kukupa taarifa muhimu zihusuzo usajili, kozi, ada na michango, anwani na huduma nyinginezo zitolewazo na kituo hiki.

 

Maulizo ote yahusuzo usajili, kozi na shughuri zote zinaofanywa na kituo yaelekezzwe kwa

 

Mkuu wa Kituo,

Kituo cha Elimu na Ushauri cha Tanganyika,

Makao Makuu,

Barabara ya Kuelekea Chuo Kikuu Cha Ardhi

Nyuma ya Hoteli ya Essaurp Village,

Eneo la Savei, Mlalakuwa (Zamani – Mlalakuwa Club)

Kitalu Namba 249/2

S. L. P3336, Da es Salaam

Tel:  +255 686 989 898

Mob +255 744 989 898

        +255 753 513 084

E- Mail.kapamakisayedenis@gmail.com

 

Karibu TECC,

 

Kituo cha Habari Elimu na Ushauri cha Tanganyika (Tanganyika Edu-Consult Centre) ni asasi isiyokuwa ya kiserikali iliyo na usajiri kamili serikalini. Moja katika malengo yake ni kupambana na adui ujinga kwa watu ambao kwasababu mbalimbali hawakupata au kukamilisha hatua mbalimbali za elimu ya sekondari. Elimu hii ya kuanzia kidato cha kwanza hadi cha sita kupitia mfumo usio rasmi hutolewa na kituo chini ya usimamizi na ushrikiano na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Wanafunzi wetu husoma kwa muda mfupi na mrefu kutegemea kiwango cha uelewa wa mlengwa. Kwa wenye uelewa wa haraka, huhitimu elimu ya kidato cha nne kwa miaka miwili na kwa wale wa kidato cha sita kwa mwaka mmoja tu kwa kufanya mitihani ya taifa ya Baraza la Mitihani Tanzania (BAMITA/NECTA) kama watahiniwa wa kujitegemea (Private Candidates)

 

TECC si kituo cha mitihani kwa hivi sasa. Hata hivyo, taasisi hi iko kwenye mchakato wa kuomba kituo cha mitihani kwa ngazi zote yaani QT, Kidato cha nne na kidato ch sita. Tunaendelea kuwasiliana na BAMITA/NECTA kupitia Taasisi ya Elimu ya Elimu ya Watu Wazima ili kukamilisha taratibu za kupata kituo cha Mitihani.

 

Mbali na shughuri za taaluma Kituo cha Habari Elimu na Ushauri cha Tanganyika kinatoa huduma za ushauri na malezi (Guidance and Counseling) bure na kwa kuzingatia maadili ya ushauri yakiwemo kutunza siri.

 

Shughuri hizi za Ushauri na taaluma zinaendeshwa hapa makao makuu Makao Makuu, Barabara ya Kuelekea Chuo Kikuu Cha Ardhi, Nyuma ya Hoteli ya Essaurp Village, Eneo la Savei, Mlalakuwa (Zamani – Mlalakuwa Club), Kitalu Namba 249/, jijini Dar es Salaam.

Malipo yanafanywa kwa fedha taslimu kituoni au kwa njia ya benki. Malipo kwa njia ya benki yafanywe kupitia akaunti ya kituo yenye jina la Tanganyika Edu- Consult Centre, Akaunti Namba 0152556699000 ya benki ya CRDB. Baada ya malipo kupitia benki, mwanafunzi au mteja aje na stakabadhi (pay slip) ya benki kituoni TECC.

 

Mwaka wa masomo unaanza tarehe 3 January na yapo madarasa ya Asubuhi (saa 2:00 – 8:00) na ya Jioni (saa 9:00–1:30). Madarasa ya Asubuhi hujaa mapema, hivyo kwa mwanafunzi anayetarajia kusoma darasa la asubuhi anashauriwa kujiunga mapema zaidi.

 

 

MAHITAJI MUHIMU

 

 

No

 

UFAFANUZI

GHARAMA Kwa Mwaka

1.

Usajili (Lazima)

Tsh. 50,000/=

2.

Usajili wa TEWW (Lazima)

50,000/=

3.

Ada ya Mwezi

50,000/=

4.

Mradi wa Vitabu

null

5.

Sare (Hiari)

50,000

6.

T-Shirts (Isiyo na kola), Hiari

       (Yenye kola), Hiar Yenye kola A)

  10,000/=

  15,000/=

 

7.

Mitihani ya Utamilifu ya TECC/TEWW

QT 10,000/=

F4 15,000/=

8.

Mitihani ya kila mwezi Sh. 5,000/=

60,000/=

9.

Safari ya kimasomo (Study Tour) 

35,000/=

10.

Tamasha la mwaka

15,000/=

11.

Mahafali F4 Sherehe ya QT

F4 25,000/=

QT 15,000/=

12.

Kitambulisho

10,000/=

 

Tanbihi: Malipo ya awali ili mwanafunzi aweze kuanza    masomo ni sh. 110,000/=

                 Ada na michango hiyo hapo juu haihusu usajili wa mitihani ya Taifa.

 

SIKU NA MUDA WA VIPINDI

SIKU

MUDA

JUMATATU-IJUMAA

ASUBUHI: SAA 2:00 – 8:00

JIONI:        SAA 9:00 – 1:30

4

·          HAKUNA MASOMO SIKU ZA SIKUKUU NA WEEK END

·          MASOMO YA O-LEVEL YANAANZA  3 January 2021

·          MASOMO A-LEVEL YANAANZA  1 MACHI 2015

 

 

 

MASOMO YANAYOFUNDISHWA

 

MASOMO

 

No

O- LEVEL

A- LEVEL

1.

CIVICS

 

2.

HISTORY

 

3.

GEOGRAPHY

H K L

4.

KISWAHILI

 

5.

ENGLISH LANGUAGE

HGK

6.

LITERATURE IN ENGLISH

 

7.

BASIC MATHS

HGL

8.

9.

10.

BIOLOGY

PHYSICS

CHEMISTRY

 

           ECA

           HGE

           PCB

           PCM

          CBG

            EGM

 

COMPUTER COURSE


FAIDA 10 ZA KUSOMA TECC

Wanafunzi wanaosoma kituo hiki hunufaika na mambo makuu kumi kama ifuatavyo:

 

1.  Wanafunzi wetu wanasoma kwenye kituo chenye kutambuliwa na Wizara ya Elimu kupitia Usajiri na Usimamizi wa Taasisi ya Elimu Ya Watu Wazima. Hii inafanya taasisi izingatie viwango vilivyowekwa na wizara ikiwemo sifa za walimu. Walimu wetu hukaguliwa na Wizara ya Elimu kupitia Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

 

2.  Wanfunzi wetu wanansajiliwa na wizara kupitia Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na hivyo hufanya mitihani ya Utamilifu ili kujipima na wanafunzi wengine nchi nzima kabla ya kufanya mitihani ya taifa.

 

3.  Wanfunzi wetu wananapewa vyeti vya kuhitimu au Leaving Certificates) zinazotolewa na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima na hivyo chini ya Wizara ya Elimu. Vyeti hivi vinatabulika na mamlaka zote nchini na nje ya nchi.

 

4.  Wahitimu wetu wa kidao cha nneambao hufaulu hupewa fursa ya kujaza fomu za kozi mbalimbali, yaani Selection Form au Sel-form na hivyo kuchaguliwa kwenda kidato chatano kwenye shule za serikali, Vyuo vya Ufundi stadi yaani VETA, Vyuo vya ualimu na Chuo cha Polisi Moshi sawa na wale wanaosoma shule za serikali.

 

5.  Wanfunzi wetu wanapata huduma ya ushauri na malezi, yaani Guidance and Counselling bure. Elimu hi inahusu mabadiriko ya mwili, Elimu ya ukimwi, Elimu ya uzazi na uchaguzi wa kozi za elimu ya juu, n.k.

 

6.  Wanfunzi wetu wanapata fursa kujifunza kwa vitendo kupitia safari za kimasomo au Study Tours, semina za wataalamu mbalimbali kutoka nyanja kadhaa kama vile siasa, michezo, mazingira, historia, sanaa, uongozi wa serikali ya wanafunzi, nk. Vile vile hii ni njia ya kutambua vipaji na mwelekeo wa kitaaluma na kimaisha.

 

7.        Wanfunzi wetu hasa wale wa QT hupewa kozi maalumu ya Kiingereza ya mizi mitatu  ili kuwasaidia wasio na msingi wa lugha hii ambayo ni ya kufundishia na kujifunzia.

 

8.        Wanafunzi wetu wanafundishwa na walimu wenye weledi, uzoefu na ari kubwa ya kujitolea. Kwa eengi wao kufundisha si ujuzi na kazi tu bali pia ni mapezi au hobby.

 

9.        TECC ni kimbilio la watu wenye uwezo mdogo kimapato. Gharama za ada na michango mingine ni ndogo na inalipwa kwa awamu (instalments). Vilevile TECC ina mpago maalumu wa kusaidia wsiojiweza kwa kuwaondolea sehemu ya ada au ada yote.

 

10.     Wanajumuiya wote wa TECC aani wanafunzi, walimu na wafanyakazi wasio walimu wanaishi kama familiya moja. Tukio la furaha au majanga linalomsibu mmoja wetu huwaungnisha wanajumuiya wote katika kulishughurikia kwa hali na mali. Tunashirikiana kwenye magonjwa, misiba, harusi, dharula za ajali, moto n.k.

 

11.     Wanafunzi wetu wanasoma kwenye kituo chenye huduma za maktaba ndogo ambayo huwapa fursa ya kuazima vitabu vya kiada na vile vya ziada.

 

12.     TECC ni kituo kinachoendeshwa kwa misingi ya democrasia kwa ktambua haja na umuhimu wa wanafunzi kuwa na serikali ya wanafunzi ambayo huwa kiungo kati ya uongozi mkuu na wanafunzi.

 

IDARA ZA KIUTENDAJI

 

Kituo cha Habari Elimu na Ushauri cha Tanganyika

(Tanganyika Edu-Consult Centre) ni asasi inayotekeleza  shughuri zake kupitia idara sita kama ifuatavyo:

1.    Idara ya Elimu: Idara hii inashughurikia na kusimamia  elimu ya sekondari na Elimu ya juu.

2.    Idara ya Malezi na Ushauri: Idara hii inashughurikia na kusimamia utoaji wa ushauri na malezi (au Guidance and Counselling)

 

3.    Idara ya Ustawi wa Jamii: Idara hii inashughurikia na kusimamia mambo yote ya kijamii yakiwemo matukio yote ya furaha au maafa yanayomkuta mwanajumuiya. Vile vile hushirikiana na mamlaka za kijamii na za kiserikali katika kutoa huduma na elimu katika majanga au maafa.

4.    Idara ya Kupambana na Umaskini: Idara hii inashughurikia shughuri zote zinazolenga kundoa umaskini hasa kupitia elimu na uhamasishaji, kufanya tafiti na harambe za kuwasaidia wenye uhitaji. 

5.    Idara ya Elimu ya Afya ya Uzazi: Idara hii inashughurikia na kusimamia utoaji wa elimu na ushaurijuu ya mambo yote yanayohusu afya ya uzazi, magonjwa ya kuambukiza na kupanga uzazi.

6.    Idara ya Elimu kwa Umma: Idara hii inashughurikia na kuratibu idara nyingine zote kwenye mambo yote yanayohitaji uhamasishaji wa umma.

 

MAFANIKIO KITAALUMA

Taasisi hii ilianzishwa kwa lengo moja kuu ambal ni kupambana na maadui wakuu watatu yaani ujinga, maradhi na umaskini. TECC inaamini kwamba mwanzo mzuri wa vita hii ni kuondoa kwanza ujinga na maadui wengine wawili wanaweza kutokomea kwa urahisi zaidi.

 

Tangia kuanzishwa kwake Aprili Mosi, 2002, TECC imefanikiwa kuwavusha maelfu ya watanzania kutoka ngazi ya elimu ya msingi na kuingia na kuhitimu elimu ya sekondari na vyuo vikuu. Na wengine kutoka elimu ya sekondari kwenda na kuhitimu ngazi ya diploma na digrii. Kila chuo kikuu cha Tanzania kumekuwepo wanafunzi ambao ni wahitimu wa kidato cha sita kutoka TECC.

 

Vile vile TECC kupitia idara ya Malezi na Ushauri imefanikiwa kuwarekebisha tabia vijana wengi na kuleta matumaini mapya kwenye family, jamii na taifa.

 

Watumishi mbalimbali wa idara za serikali wakiwemo walimu, wauguzi , askari  polisi katika mkoa wa Dar es Salaam wamesomea TECC . Wengine ni wafanyabiashara/wajasiliamali, mama wa nyumbali watumishi wa ndani, n.k.wamesomea TECC na kubadilisha historia zao za maisha.

 

Karibu katika ulimwengu wa taaluma ili kutimiza ndoto yako. Tumekusudia na kujipanga vyema kubadili historia na wasifu wako.

ELIMU NI RASILIMALI NA URITHI BORA

 


Post a Comment

0 Comments